Posts

Showing posts from March, 2017

JINSI YA KUPIKA KUKU NA NDIZI ZA MSHALE

Image
KUKU NA NDIZI MSHALE NI SAFI SANA KWA MLO KAMILI USIKU AU MCHANA PIA UNAWEZA WEKA KARANGA AU TUI LA NAZI. KARIBU JIFUNZE KUPIKA KWA KUFUATA MAELEKEZO HAPA CHINI   Kwa ndugu zangu mliopo ughaibuni ndizi si nzuri san kama ndizi inayotoka Moshi, Arusha au bukoba kwahiyo njia hii ya upishi itakufanya ufurahie sana na usione tofauti ya ladha na kula ndizi laini na safi kabisa Menya ndizi zako kisha zipake mafuta ya kupikia na chumvi kisha ziweke kwenye oven kwa dakika 15 hadi 20 zitakua zimeiva na laini za kutosha Pia kuku ipake kitunguu swaumu, pili pili manga, chumvi kisha iweke kwenye oven bila maji itajipika safi na kutoa mchiz kiasi pia utautumia kwenye pishi lako la ndizi oven inasaidia kupika vizuri bila nyama kurojeka na hupotezi vile viuongo kama huna one basi chemsha katika sufuri kwa moto mdogo bila ya kuweka maji ili maji yatakayojichuja toka kwa kuku yataweza kuivisha nyamachunga yasikauke. Weka kitunguu ...

JIFUNZE KUTENGENEZA CAKE

Image
Mapishi ya keki Siku zote mtu anatakiwa awe mbunifu kwa kila kitu.Ila leo nagusia upande wa jikoni.Kwa upande wa wanawake katika sekta nzima ya maakuli mambo ya jikoni shuti unatakiwa uwe mtundu,leo unabuni hiki na kesho unafanya vile ili mradi uweze kupata vionyo tofauti tofauti.Raha ya chakula shuti upike mwenyewe bibi..'mwanamke jiko eeh''. Leo tutaangalia namna ya kupika keki ya kawaida hasa ukiwa nyumbani.Karibuni tujifunze pamoja Mahitaji: Unga wa ngano glasi 4 Mayai 10 Sukari glasi 3 Baking powder vijiko 2 vya chai Unga wa mdalasini kijiko 1 cha chai Zabibu kavu Maziwa fresh 1/2 glasi na mtindi 1/2 glasi Cocoa au kahawa Vanila tui la nazi zito kabisa,kiasi Mafuta 1/4 lt Tray ya kuokea keki yako Sufuria/chombo cha kuchanganyia mchanganyiko wako Hatua za kupika: Tayarisha oven yako kwa kuiwasha katika moto wa nyuzi 185 sentigrade (365F) Paka mafuta kiasi kwenye kikaangio/tray yako kisha kiweke pembeni Pasua mayai yako kisha yaweke tkt '...

JINSI YA KUPIKA WALI WA BIRYAN YA KUKU, NG.OMBE AU MBUZI

Image
Mahitaji 1 kilo mchele wa basmati mrefu 1 kilo nyama iwe ya kuku au ng'ombe au mbuzi kata katika umbo dogo la kutosha kula kisha ichemshe na tangawizi na kitunguu swaumu, unga wa binzari (turmeric powder) pili pili manga na chumvi ili kuweka ladha nzuri. Ikisha iva itoe iweke pembeni na mchuzi wake uweke pembeni utautumia baadae. 1 kilo ya vitunguu kata slice ( mviringo) 1 kilo nyanya nyekudu zilizoiva, osha vizuri kisha katakata saizi ndogo ndogo sana 240 gram ya mafuta ya kupikia 240 gram ya samli au mafuta yeyote ya kupikia 2 maggi chicken soup cubes 3 kijiko kidogo cha chai unga wa pilipili mwekundu 1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa binzari (turmeric powder) 3 kijiko kidogo cha chai unga wa girigilani (coriander powder) 2 kijiko kikubwa cha chakula mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu swaumu vilivyosagwa (ginger-garlic paste ) 50 gram korosho iliyo kaangwa usizisage zibaki nzima 50 gram majani ya girigilani (fresh coriander leaves, washed and chopped) 8-12 mbegu...

Nyama ya ng'ombe ya kukaanga yenye utamu wa kipekee

Image
Mahitaji Nyama  - kilo 1 Mafuta ya kula - 1/2 lita Chumvi Ndimu (Limao au vinegar) 1 Tangawizi  - 1 Kitunguu saumu  - 1 Cube magic Viazi - 6 Viungo vingine upendavyo kwenye sauce*. Maelekezo Tayarisha nyama yako - kata, osha. Weka limao, ndimu au vinegar kwenye nyama, ichanganye ili limao lichanganyike vizuri. Ponda tangawizi kwenye kinu, iwe laini. Ponda kitunguu swaumu kwenye kinu, ilainike vizuri. Weka viungo - chumvi, cube maggie, tangawizi na kitunguu saumu kwenye nyama. Changanya nyama ili viungo vipate kuchanganyika vizuri. Acha nyama ikae kwa dakika 40 kwenye jokofu ili viungo viingie vizuri. Jinsi viungo vinavyokaa vizuri kwenye nyama ndio inazidi kunoga. Bandika sufuria au kikaangio jikoni, weka mafuta kiasi. Subiria yapate moto. Weka nyama kwenye mafuta.  Koroga ili ichanganyike vizuri na mafuta kisha funika sufuria au chungu na mfuniko. Fanya hivi ili kuiacha nyama ikaangwe na mafuta lakini inaiva na mvuke wake pia. Geuza geuza nyama kil...